KIMBUNGA MARIA KIMESABABISHA VIFO VYA WATU 7 HUKO PUERTO RICO.



TAREHE 21-09-2017

MADHARA  YA KIMBUNGA  MARIA 

Kimbunga Maria kimekata umeme katika kisiwa chote cha Puerto Rico, chenye watu milioni 3.5  huku kikiwa tayari kimesababisha vifo vya watu 7 katika kisiwa cha Dominica ambacho kiliathiriwa vibaya siku ya Jumatatu.


Abner Gómez, ambaye ni mkuu wa utoaji huduma za dharura alisema kuwa hakuna mtu anayetumia umeme aliye na huduma hiyo hadi sasa.
Kituo cha vimbunga cha Marekani kinasema kuwa mafuriko makubwa yanaikumba nchi hiyo.

Kimbunga Maria kwa sasa kinaondoka nchini Puerto Rico na kumepunguza nguvu zake hadi kiwango cha pili.


Baada ya kimbunga Maria kuipiga Puerto Rico, gavana ameamrisha watu kusalia manyumbani mwao kuanzia saa kumi na mbili jioni hadi saa kumi na mbili asubuhi.
KIMBUNGA MARIA KIMESABABISHA VIFO VYA WATU 7 HUKO PUERTO RICO. KIMBUNGA  MARIA  KIMESABABISHA  VIFO  VYA  WATU   7  HUKO   PUERTO RICO. Reviewed by safina radio on September 21, 2017 Rating: 5

No comments