WABUNGE WA UGANDA WAMEPIGANA NDANI YA UKUMBI WA BUNGE

TAREHE 28-09-2017



Wabunge nchini Uganda wamepigana ndani ya ukumbi wa bunge wakiwa katika siku ya pili ya kikao cha kujadiliwa mswada wa kuondoa ukomo wa miaka ya kugombea nafasi ya urais kwa mujibu wa katiba ya taifa hilo.

katika kikao hicho kilichoongozwa na Spika wa bunge, Bi.Rebecca Kadaga wabunge walirushiana viti, na kuharibu vipaza sauti.

Ugomvi huo ulianza pale Spika alipochukua hatua ya kuwafukuza wabunge wapatao 25 wengi wao wakiwa ni wa upinzani kwa madai ya utovu wa nidhamu pamoja na waziri wa serikali aliyeshtakiwa kwa kufyatua risasi bungeni siku ya jumanne.


Wabunge hao wanadai kuwa kama kikomo cha umri wa miaka 75 kitaondolewa basi rais aliyepo madarakani kwa sasa atapata mwanya wa kugombea tena mwaka 2021.
WABUNGE WA UGANDA WAMEPIGANA NDANI YA UKUMBI WA BUNGE WABUNGE    WA  UGANDA  WAMEPIGANA  NDANI YA  UKUMBI  WA BUNGE Reviewed by safina radio on September 28, 2017 Rating: 5

No comments