KIONGOZI WA MYANMAR AHUTUBIA TAIFA NA KUZUNGUMZIA GHASIA NCHINI HUMO.
TAREHE 19-09-2017
![]() |
KIONGOZI WA MYANMAR AUNG SAN SUU KYI |
Kiongozi
wa Myanmar, Aung San Suu Kyi amelihutubia taifa ambapo amezungumzia ghasia
zinazoendelea nchini humo dhidi ya ya Waislamu wa Rohingya katika jimbo la
Rhakine.
Akizungumza
kwa mara ya kwanza tangu kuzuka kwa ghasia hizo mwezi uliopita, Aung San Suu
Kyi amesema serikali yake inalaani vikali ukiukwaji wa haki za binaadamu na
unyanyasaji unaofanywa kinyume cha sheria.
Amesema wako tayari kuanza mchakato wa
kuwarejesha nyumbani wakimbizi wowote ambao wanataka kurejea nchini humo baada
ya kukimbilia nchi jirani ya Bangladesh.
Suu
Kyi mwenye umri wa miaka 72, na mshindi wa tuzo ya amani ya Nobel ameitoa
hotuba hiyo baada ya mataifa yenye nguvu duniani kuionya Myanmar kwamba inaweza
ikakabiliwa na hatua, iwapo haitachukua hatua za kukomesha ukandamizaji
unaofanywa dhidi ya jamii ya watu wachache wa Rohingya katika jimbo la Rakhine.
KIONGOZI WA MYANMAR AHUTUBIA TAIFA NA KUZUNGUMZIA GHASIA NCHINI HUMO.
Reviewed by safina radio
on
September 19, 2017
Rating:

No comments