WATANZANIA WAMETAKIWA KUWA NA TABIA YA KUOMBEA FIKRA ZAO KWA LENGO LA KUKOMBOA MAJIRA NA NYAKATI.


TAREHE 15-09-2017



Watanzania wametakiwa kuwa na tabia ya kuombea fikra zao ili kukomboa majira na nyakati pamoja na vitu vilivyokufa kiroho na kimwili kwani watu wengi wamekuwa wakijushughulisha na kazi bila kufikia mafanikio.

Aidha katika mwendelezo wa maombi ya ili kukombolewa  kifikra pamoja na majira na nyakati za mtu zilizokufa,redio safina kesho katika ukumbi ulioko mbauda jijini Arusha itajikita katika kufundisha watu jinsi ya kukomboa  fikra zao katika ulimwengu wa  roho ili kila mmoja ajue ni namna gani ataweza kukomboa uhai wa vitu vilivyokufa kiroho.

Katika kuyabainisha mambo yanayoweza kufa imebainika kuwa ni pamoja na elimu biashara,kilimo na ufugaji,tumbo la uzazi, ndoa, huduma na miradi mingine ambapo kesho maombi ya nguvu yatafanyika ili kuyavika uhai.

Sambamba na maombezi kufanyika watu wote wanashauriwa kuja na vielelezo vya kazi zao pamoja na chumvi ambapo vitu hivyo vitaombewa kwa kitendo cha imani cha kuyavika uhai ili kila mmoja aweze kufikia mafanikio aliyojiwelea.


Hata hivyo iwapo mtu atashindwa kukomboa fikra,majira na nyakati zake ni vigumu kumtumikia Mungu wala kufanikiwa kwenye shughuli yoyote.
WATANZANIA WAMETAKIWA KUWA NA TABIA YA KUOMBEA FIKRA ZAO KWA LENGO LA KUKOMBOA MAJIRA NA NYAKATI. WATANZANIA  WAMETAKIWA  KUWA  NA  TABIA  YA  KUOMBEA  FIKRA ZAO  KWA   LENGO  LA  KUKOMBOA  MAJIRA  NA  NYAKATI. Reviewed by safina radio on September 15, 2017 Rating: 5

No comments