WAKULIMA WATAKIWA KUFUATA USHAURI UNAOTOLEWA NA WATAALAM


Wakulima hapa nchini wametakiwa kufuata ushauri unaotolewa na wataalamu wa kilimo pale wanapoanza msimu wa kilimo  ili waweze kujua njia bora za kuzalisha mazao yao.

Image result for PICHA YA MAHARAGE SHAMBANI


Ushauri huo umetolewa na Bi Edith Kadege mtaalamu wa wadudu na magonjwa ya mazao  kutoka kituo cha utafiti wa kilimo Seliani Arusha wakati akizungumza na Redio Safina kuhusu changamoto mbalimbali zinazowakabili wakulima hasa kipindi hiki cha msimu wa kilimo.

Bi Kadege amesema kuwa wakulima wengi wanapoanza kilimo chao wamekuwa wakilima kilimo cha mazoea badala ya kuchukua maelezo yanayotolewa na wataalamu wa kilimo hususani njia bora ya kuandaa mashamba yao ambayo ndio njia mojawapo itakayomsaidia mkulima kupata mazao mengi.

Katika eneo la upatikanaji wa mbegu bora mtaalamu huyo amesema kuwa kituo cha utafiti Seliani kimekuwa kikifanyia utafiti mbegu mbalimbali ikiwemo Maharage na Mahindi kwa kuwa ndio mazao makuu yanayolimwa na wananchi hivyo ni vyema wakulima wakafika katika kituo hicho pamoja na wakala wa uuzaji wa mbegu ASA ili kupata mbegu hizo.

Hata hivyo amewataka wakulima wanapokuwa na shida inayohusiana na kilimo kuwasiliana na vituo vya utafiti vilivyoko katika maeneo yao ikiwemo cha kanda ya kaskazini Seliani,Sua Morogoro na mkoani Tanga.

WAKULIMA WATAKIWA KUFUATA USHAURI UNAOTOLEWA NA WATAALAM WAKULIMA WATAKIWA KUFUATA USHAURI UNAOTOLEWA NA WATAALAM Reviewed by safina radio on April 02, 2018 Rating: 5

No comments