MBUNGE WA CHAMA TAWALA CHA JUBILEE ATAKA JAJI MKUU NCHINI KENYA KUFUTWA KAZI

TAREHE 14-09-2017

JAJI MKUU WA KENYA DAVID MARAGA

Mbunge wa chama tawala cha Jubilee nchini Kenya amewasilisha ombi la kutaka kufutwa kazi kwa jaji mkuu David Maraga.
Mbunge huyo wa Nyeri, Njiri Wambugu amewasilisha ombi lake mbele ya tume ya huduma za majaji akidai kwamba jaji Maraga alihusika katika kufanya makosa ya kutengua ushindi wa rais Uhuru Kenyata.
Akihutubia vyombo vya habari, mbunge huyo amedai kwamba Jaji huyo ''aliwashinikiza'' wenzake kubatilisha matokeo ya uchaguzi wa rais Uhuu Kenyatta wakati alipotoa uamuzi wa kihistoria mnamo tarehe 1 Septemba mwaka huu mwaka huu.
Wambugu amefananisha ubatilishwaji wa matokeo hayo ya urais na mapinduzi ya majaji na sasa anataka nia ya jaji Maraga kuchunguzwa.

Wabunge wa chama cha Jubilee na rais Uhuru Kenyatta wamekuwa wakiukosoa uamuzi wa kufutilia mbali uchaguzi huo na wameendelea na kuwataja majaji hao kuwa ''wakora''.
MBUNGE WA CHAMA TAWALA CHA JUBILEE ATAKA JAJI MKUU NCHINI KENYA KUFUTWA KAZI MBUNGE WA CHAMA TAWALA CHA JUBILEE ATAKA JAJI MKUU NCHINI KENYA KUFUTWA KAZI Reviewed by safina radio on September 14, 2017 Rating: 5

No comments