MHANDISI WA MAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MBINGA ASHIKILIWA POLISI KWA UBADHIRIFU WA FEDHA ZA MRADI


tarehe 21-09-2017


KAMANDA WA POLISI MKOA WA RUVUMA GERMIN MUSHI

Jeshi la polisi katika wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma linamshikia mhandisi wa maji wa halmashauri ya wilaya ya Mbinga Bi Vivian Ndolwa kwa tuhuma za kuhusika na ubadhirifu wa fedha za mradi wa maji zaidi ya shilingi milioni mia saba.

Akidhibitisha kushikiliwa kwa mahandisi huyo kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Ruvuma SACP Germin Mushi amesema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa Sept 19 mwaka huu,ambapo amesema kuwa mhandisi huyo alikuwa akisimamia mradi wa maji wa katika kitongoji cha Mnazi mmoja kijiji cha Mkako kata ya Mkako mmkoani humo.

Kamanda Mushi amesema kuwa,mradi huo unaofadhiliwa na benki ya dunia ulitakiwa kukamilika March 28 2014 lakini hadi sasa mradi huo haujakamilika na umejengwa chini ya kiwango hivyo wameamua kumkamata ili akjibu tuhuma hizo zinazomkabili.


Hata hivyo amesema baada ya kukamilika kwa upelelezi jalada la kesi litapelekwa kwa mwanasheria wa serikali wa mkoa wa Ruvuma kwa hatua zaidi.
MHANDISI WA MAJI HALMASHAURI YA WILAYA YA MBINGA ASHIKILIWA POLISI KWA UBADHIRIFU WA FEDHA ZA MRADI MHANDISI    WA   MAJI   HALMASHAURI   YA  WILAYA   YA  MBINGA  ASHIKILIWA   POLISI   KWA   UBADHIRIFU    WA  FEDHA   ZA  MRADI Reviewed by safina radio on September 21, 2017 Rating: 5

No comments