ROONEY AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KOSA LA KUENDESHA GARI AKIWA AME LEWA
TAREHE 18-09-2017
![]() |
WAYNE ROONEY |
Nahodha wa zamani wa
kikosi cha England Wayne Rooney amefika mahakamani na kukiri kuendesha gari
akiwa mlevi.
Alikamatwa wakati
polisi walisimamisha gari lake huko Wilmslow, Cheshire tarehe mosi mwezi
Septemba.
Rooney 31 alipigwa
marufuku ya kuendesha gari kwa miaka miwili na kuamrishwa kutoa huduma ya jamii
bila malipo kwa masaa 100.
Rooney pia aliamrishwa
kulipa pauni 170 wakati alifika katika mahakama ya Stockport.
Mzaliwa huyo wa
Liverpool aliyejiunga tena na klabu yake ya utotoni ya Eveton miaka 13 tangu
akihame na kuelekea Manchester United.
Baba huyo wa watoto
watatu ndiye anayeshikisa rekodi ya kufunga mabao mengi zaidi nchini Uingereza.
ROONEY AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KOSA LA KUENDESHA GARI AKIWA AME LEWA
Reviewed by safina radio
on
September 18, 2017
Rating:

No comments