IMEELEZWA KUWA VITENDO VYA RUSHWA VINAENDELEA KUPUNGUA HAPA NCHINI
TAREHE 21-09-2017
![]() |
NAIBU MKURUGENZI TAKUKURU BRIGEDIA JENERALI JOHN MBUNGO |
Naibu
mkurugenzi mkuu wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) hapa
nchini, Brigedia Jenerali John Mbungo amesema kuwa vitendo vya rushwa
vinaendelea kupungua hapa nchini kutokana na juhudi kubwa zinazofanywa na
taasisi hiyo ya kuwakamata na kuwachukulia hatua wala rushwa.
Jenerali
Mbungo ameyasema hayo jijini Dar-es-salaam,wakati akifungua mafunzo ya namna ya
kuzuia na kupambana na rushwa kwa viongozi wa serikali za mitaa na wakurugenzi
wa taasisi na mashirika mbalimbali ya mkoa wa Dar-es-salaam ambamo ndipo
panapofanyika shughuli nyingi za wananchi.
Amesema kuwa
mafunzo hayo ni mwendelezo wa utaratibu wa takukuru ya kuwafundisha watoa
huduma namna ya kuzuia na kupambana na rushwa katika maeneo yao ya kazi ikiwemo
polisi na mahakamani,hivyo baada ya mafunzo hayo wanaamini kuwa rushwa
itapungua kwa kiasi kikubwa katika maeneo mbalimbali ya kuhudumia wananchi hapa
nchini.
Kwa upande
wake katibu tawala wa mkoa wa Dar-es-salaam Bi Theresia Mbando amesema
kuwa,katika mkoa huo vitendo vya rushwa vimepungua katika maeneo ya kutolea
huduma,ambapo pia amewataka watoa huduma wa mkoa huo kuzingatia maadili ya kazi
na kujiepusha na vitendo vya rushwa.
IMEELEZWA KUWA VITENDO VYA RUSHWA VINAENDELEA KUPUNGUA HAPA NCHINI
Reviewed by safina radio
on
September 21, 2017
Rating:

No comments