WAMAMA WAJAWAZITO 100 WAMEFARIKI DUNIA MKOANI MWANZA TANGU MWEZI JANUARI HADI AGOSTI MWAKA HUU
TAREHE 20-09-2017
![]() |
BAADHI YA WAMAMA WAJAWAZITO WAKIWA KATIKA KITUO CHA AFYA |
Imeelezwa
kuwa Jumla ya wamama wajawzito 100 wamefariki dunia mkoani Mwanza kuanzia mwezi
Januari hadi mwezi Agosti mwaka huu kutokana na matatizo ya uzazi
ikilinganishwa na vifo vya akina mama wajawazito 80 waliofariki dunia mwaka
jana katika kipindi kama hicho.
Hayo
yameelezwa na mratibu wa afya wa mama na mtoto mkoani Mwanza Bi Cesilia
Mrema,ambapo amesema kuwa vifo hivyo ni ongezeko kutoka 494 kwa mwaka wa 2012
hadi vifo 556 katika vizazi hai laki moja kwa mwaka huu,hivyo juhudi zaidi
zinahitajika ili kupunguza vifo hivyo.
Aidha mradi
wa mama na mtoto unaolenga kupunguza vifo vya akina mama wajawazito na watoto
unatekelezwa katika wilaya za Kwimba na Misungwi mkoani Mwanza,ambapo zitatatuliwa
changamoto mbalimbali ikiwemo ujenzi wa hodi za wazazi.
Hata hivyo
azma ya serikali ya awamu ya tano ni kuhakikisha kuwa inapunguza vifo
vitokanavyo na uzazi ambapo serikali imekuwa ikitumia njia mbalimbali ili
kuhakikisha tatizo hilo linapungua,ikiwemo kutoa elimu juu ya umuhimu wa akina
mama wajawazito kujifungulia katika vituo vya afya pamoja na kujenga hodi za
akina mama wanaojifungua.
WAMAMA WAJAWAZITO 100 WAMEFARIKI DUNIA MKOANI MWANZA TANGU MWEZI JANUARI HADI AGOSTI MWAKA HUU
Reviewed by safina radio
on
September 20, 2017
Rating:

No comments