MKE WA WAZIRI MKUU WA PAKISTAN ALIYEONDOLEWA MADARAKANI NAWAZI SHARIF,ASHINDA KUWANIA UBUNGE


TAREHE 18-09-2017

KULSOOM  NAWAZ 
Mke wa Waziri mkuu wa Pakistan aliyeondolewa Madarakani Nawaz Sharif, ameshinda katika kuwania kiti cha ubunge kilichoachwa na mumewe kwenye uchaguzi uliofanyika Lahore, jimbo mbalo ni ngome ya familia yao.
Matokeo yasiyo rasmi yanaonesha kuwa Kulsoom Nawaz amemshinda mpinzani wake, kwa kura chache.
Kura hizo zinaonesha kama ni jaribio la kumuunga mkono kiongozi wa chama cha Pakistan Muslim League Nawaz Sharif, wakati katika kukikaribia uchaguzi mkuu wa mwaka ujao.
Waziri mkuu huyo wa zamani alienguliwa madarakani na mahakama kuu nchini humo mwezi Julai,kufuatia tuhuma za rushwa.

Hata hivyo mshindi wa kiti hicho Kulsoom Nawaz kwa sasa yuko mjini London kupata matibabu ya ugonjwa wa saratani.
MKE WA WAZIRI MKUU WA PAKISTAN ALIYEONDOLEWA MADARAKANI NAWAZI SHARIF,ASHINDA KUWANIA UBUNGE MKE  WA  WAZIRI  MKUU  WA  PAKISTAN ALIYEONDOLEWA  MADARAKANI  NAWAZI  SHARIF,ASHINDA  KUWANIA  UBUNGE Reviewed by safina radio on September 18, 2017 Rating: 5

No comments