SUMATRA MKOA WA PWANI KUWAPELEKA MAHAKAMANI MADEREVA WA MAGARI YA ABIRIA AINA KOSTA NA HIECE YASIYOPITA KATIKA KITUO CHA LOLIONDO KIBAHA

TAREHE  27-09-2017

Mamlaka ya udhibiti wa usafiri wa nchi kavu na majini SUMATRA mkoa wa Pwani imesema kuwa itawapeleka mahakamani pamoja na kuwafungia leseni madereva wa magari ya abiria aina ya Kosta na hiece asiyopita katika kituo cha Loliondo Kibaha mkoani Pwani.

Hayo yameelezwa na afisa mfawidhi wa Sumatra mkoa wa Pwani Bw Omary Ayubu katika zoezi la ukaguzi wa magari aina ya kosta yanayofanya safari zake kati ya Mbezi na Mlandizi mkoani humo.

Amesema kuwa mamlaka hiyo haitawafumbia macho madereva wanaokataa kupitia katika kituo cha loliondo kwa kuwa ndicho kituo cha mabasi madogo na kama kuna malalamiko yafikishwe katika ofisi za SUMATRA badala ya kugoma na kuwanyima haki ya kusafiri abiria.

Kwa upande wake kamanda wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Pwani Bw Salim MoriMori ametoa wito kwa wamiliki wa mabasi kuhakikisha wanaboresha vyombo vyao vya moto ili kukidhi viwango vya usafirishaji.


Hata hivyo Bw MoriMori amesema wameamua kufanya operesheni ya kustukiza kwa kushirikiana na SUMATRA ili kuwajengea madereva kumbukumbu ya kusimamia na kufuata sheria za usalama barabarani,ambapo katika operesheni hiyo wamefanikiwa kukamata magari 14 ya abiria yaliyokuwa na makosa mbalimbali ikiwemo kika sheria za usalama barabarani.
SUMATRA MKOA WA PWANI KUWAPELEKA MAHAKAMANI MADEREVA WA MAGARI YA ABIRIA AINA KOSTA NA HIECE YASIYOPITA KATIKA KITUO CHA LOLIONDO KIBAHA SUMATRA  MKOA   WA  PWANI    KUWAPELEKA    MAHAKAMANI   MADEREVA   WA MAGARI  YA   ABIRIA   AINA    KOSTA  NA   HIECE     YASIYOPITA   KATIKA  KITUO  CHA   LOLIONDO    KIBAHA Reviewed by safina radio on September 27, 2017 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.