BARAZA LA USALAMA LA UMOJA WA MATAIFA LAELEZA WASIWASI WAKE KUHUSU NGUVU ZINAZAZOTUMIWA NA MYANMAR





KATIBU MKUU WA UMOJA WA MATAIFA KUSHOTO ANTONIO GUTTERES


Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limeelezea wasiwasi wake kuhusu nguvu ya kupita kiasi zinazotumiwa na Myanmar wakati wa operesheni yake ya usalama katika jimbo la Rakhine na limetaka hatua za haraka zichukuliwe kukomesha machafuko hayo.

Taarifa ya pamoja iliyotolewa baada ya kikao cha faragha cha baraza hilo kujadili machafuko ya Myanmar ambayo yamewalazimu waislamu wa jamii ya Rohingya takriban laki tatu na themanini  kuvuka mpaka na kukimbilia nchi jirani ya Bangladesh.

Baraza hilo la usalama limelaani vikali machafuko hayo na kutoa wito wafanyakazi wa kutoa misaada ya kibinadamu waruhusiwe kuwafikia watu wanaohitaji msaada katika jimbo la Rakhine.


Awali katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa mwito wa operesheni ya kijeshi katika jimbo hilo ikome mara moja na kudokeza kwamba kuhamishwa kwa lazima kwa warohingya ni safisha safisha ya kikabila.
BARAZA LA USALAMA LA UMOJA WA MATAIFA LAELEZA WASIWASI WAKE KUHUSU NGUVU ZINAZAZOTUMIWA NA MYANMAR BARAZA LA USALAMA LA UMOJA WA MATAIFA LAELEZA WASIWASI WAKE KUHUSU NGUVU ZINAZAZOTUMIWA  NA MYANMAR Reviewed by safina radio on September 14, 2017 Rating: 5

No comments