Makamu wa rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania amesema kuwa serikali ya awamu ya tano imefanya juhudi kubwa katika kuhakikisha sekta ya kilimo inatoa mchango mkubwa katika maendeleo ya jamii na kiuchumi hapa nchini.


TAREHE 6 SEPTEMBA 2017


MAKAMU WA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MH SAMIA SULUHU HASSANI
Makamu wa rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania amesema kuwa serikali ya awamu ya tano imefanya juhudi kubwa katika kuhakikisha sekta ya kilimo inatoa mchango mkubwa katika maendeleo ya jamii na kiuchumi hapa nchini.
Mh Suluhu ameyasema hayo jijini Dar-es-salaam katika maadhimisho ya miaka 40 ya ushirikiano kati ya shirika la chakula la umoja wa mataifa FAO  na Tanzania,ambapo amesema kuwa moja ya juhudi hizo za serikali ni kuondoa kodi zote zilizokuwa zikirudisha nyuma maendeleo ya wakulima nchini.Kwa upande wake waziri wa kilimo,mifugo na uvuvi Mh Charles Tizeba amesema kuwa shirika la chakula duniani limekuwa na mchango mkubwa kwa Tanzania kwa kutoa utaalamu wa namna ya kukuza sekta ya kilimo hapa nchini.Naye mkurugenzi mkuu wa shirika hilo Dr Josee Graziano Dasliva amesema kuwa shirika hilo litaendelea kushirikiana na serikali katika uboreshaji wa sekta ya kilimo na upatikanaji wa chakula salama kwa wananchi.
Makamu wa rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania amesema kuwa serikali ya awamu ya tano imefanya juhudi kubwa katika kuhakikisha sekta ya kilimo inatoa mchango mkubwa katika maendeleo ya jamii na kiuchumi hapa nchini. Makamu wa rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania amesema kuwa serikali ya awamu ya tano imefanya juhudi kubwa katika kuhakikisha sekta ya kilimo inatoa mchango mkubwa katika maendeleo ya jamii na kiuchumi hapa nchini. Reviewed by safina radio on September 06, 2017 Rating: 5

No comments