JESHI LA POLISI MKOANI KAGERA LAKAMATA MAGUNIA 57 YA BANGI


TAREHE 19-09-2017


BANGI IKIWA IMEHIFADHIWA KWENYE MAGUNIA

Jeshi la polisi mkoani Kagera limefanikiwa kukamata magunia 57 ya bangi yaliyokuwa yamehifadhiwa katika ghala la mkulima mmoja katika kijiji cha Mtoke toke wilayani Ngara mkoani humo.

Kwa mujibu wa kamanda wa jeshi la polisi mkoani Kagera Agostino Olomi amesema kuwa magunia hayo ya bangi yamekamatwa katika ghala la Bw Saimon Charles baada ya msako uliofanywa na jeshi la polisi mkoani humo.

Kamanda Olomi amesema kuwa,baada ya magunia hayo kukamatwa mtuhumiwa amekiri kujishughulisha na kilimo hicho cha bangi,na atafikishwa mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika.


Hata hivyo kukamatwa kwa magunia hayo ya bangi kumetokana na operesheni iliyofanywa na jeshi hilo na kushirikisha vikosi vya polisi vya mikoa ya kagera,Geita na kigoma.
JESHI LA POLISI MKOANI KAGERA LAKAMATA MAGUNIA 57 YA BANGI JESHI  LA  POLISI  MKOANI   KAGERA   LAKAMATA   MAGUNIA  57  YA  BANGI Reviewed by safina radio on September 19, 2017 Rating: 5

No comments