WAOKOAJI HUKO MEXICO WANAJARIBU KUMUOKOA MSICHANA ALIE HAI CHINI YA KIFUSI





TAREHE  21-09-2017
WAOKOAJI  KATIKA  MJI MKUU WA MEXICO, MEXICO CITY

Waokoaji katika mjini wa Mexico city wanajaribu kumfikia msichana mdogo, aliye hai chini ya kifusi cha jengo la shule, lililoporomoka wakati wa Tetemeko la ardhi lililotokea jana.

Waokoaji hao wamekuwa wakimpitishiamtoto huyo chakula na maji, wakati wakijaribu kutafuta njia ya kuweza kumtoa akiwa salama kutoka kwenye kifusi hicho.

Hadi sasa watoto wapatao 21 wamekufa baada ya jengo walilokuwamo kuvunjika, huku wengine wakiwa bado ndani ya kifusi hicho.
Jumla ya watu zaidi ya mia mbili wamefariki dunia kutokana na tetemeko hilo.

Rais wa Mexico Enrique Pena Nieto amesema kila dakika imekuwa ikihesabika katika kuokoa maisha.

Tetemeko hilo la ardhi ni la pili kuipiga nchi hiyo mwezi huu.
WAOKOAJI HUKO MEXICO WANAJARIBU KUMUOKOA MSICHANA ALIE HAI CHINI YA KIFUSI WAOKOAJI   HUKO   MEXICO  WANAJARIBU   KUMUOKOA  MSICHANA  ALIE  HAI  CHINI  YA  KIFUSI Reviewed by safina radio on September 21, 2017 Rating: 5

No comments