WILAYA YA MONDULI KUBORESHA MAHUSIANO KATI YA KAMBI YA JKT MAKUYUNI NA WANANCHI WANAOZUNGUKA KAMBI HIYO

TAREHE 26-09-2017
MKUU WA WILAYA YA MONDULI IDD KIMANTA

Mkuu wa wilaya ya Monduli mkoani Arusha Bw Idd Kimanta amesema kuwa,wilaya hiyo itatoa ushirikiano na kuboresha mahusiano mazuri kati ya kambi ya JKT Makuyuni na jamii inayozunguka kambi hiyo.

Bw Kimanta ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa kambi ya  kikosi namba mia nane thelathini na tisa KJ kilichopo wilayani Monduli ambapo amesema kuwa ushirikiano kati ya kambi za jeshi na wananchi unaleta mahusianao mazuri hivyo atashirikiana na viongozi wengine pamoja na wananchi ili kuhakikisha uhusiano huo unaendelea kuimarika.


Kwa upande wake mkuu wa jeshi la kujenga taifa JKT Meja Jenerali Michael Issa Moyo amewataka wakuu wa kambi hiyo kuboresha mafunzo yenye ubunifu yatakayosaidia kujifunza uzalishaji na kusaidia sera ya uchumi wa viwanda ikiwemo uzalishaji wa bidhaa mbalimbali.
WILAYA YA MONDULI KUBORESHA MAHUSIANO KATI YA KAMBI YA JKT MAKUYUNI NA WANANCHI WANAOZUNGUKA KAMBI HIYO WILAYA  YA  MONDULI   KUBORESHA  MAHUSIANO  KATI  YA  KAMBI  YA JKT MAKUYUNI  NA WANANCHI   WANAOZUNGUKA   KAMBI  HIYO Reviewed by safina radio on September 26, 2017 Rating: 5

No comments