SERIKALI KUENDELEA KUPELEKA FEDHA KWENYE SEKTA YA MAJI HAPA NCHINI


TAREHE 21-09-2017

WAZIRI MKUU WA TANZANIA MAJALIWA KASSIM MAJALIWA KUSHOTO  AKISALIMIANA NA WANANCHI

Waziri mkuu wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh majaliwa Kassimu Majaliwa amesema kuwa serikali itaendelea kupeleka fedha nyingi kwenye sekta ya maji ili kuhakikisha kuwa tatizo la maji linamalizika hapa nchini.

Mh Majaliwa ameyasema hayo leo wilayani Longido mkoani Arusha wakati wa sherehe ya uwekaji wa jiwe la msingi wa mradi wa maji wenye thamani ya shilingi bilioni 16 utakaohudumia wananchi wa wilaya hiyo,ambapo amesema kuwa lengo la serikali ni kuhakikisha kuwa mwananchi hatembei zaidi ya mita mia nne kupata huduma ya maji.

Amesema kuwa wilaya ya Longido ina upungufu mkubwa wa maji na hiyo inatokanana jiografia ya eneo hilo kuwa kame hivyo serikali itaendelea kutenga bajeti kubwa zaidi ili wananchi wote wa Longido wapate huduma ya maji ambapo kwa mwaka huu serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni mia sita kwa ajili ya miradi hiyo.

Kwa upande wake waziri wa maji na umwagiliaji Mh Gerson Lwenge amesema kuwa mradi huo wa maji utakapokamilika utawanufaisha wananchi wa vijiji vitano vya wilaya hiyo na maji yake yatatoka katika chanzo cha maji cha mlima Kilimanjaro .

Ameongeza kuwa,wizara yake ina mikakati ya kuhakikisha upatikanaji wa maji unakuwa asilimia 95 kwa mijini na 85 kwa vijijini ufikapo mwaka wa 2025.
SERIKALI KUENDELEA KUPELEKA FEDHA KWENYE SEKTA YA MAJI HAPA NCHINI SERIKALI  KUENDELEA  KUPELEKA  FEDHA  KWENYE  SEKTA   YA MAJI HAPA   NCHINI Reviewed by safina radio on September 21, 2017 Rating: 5

No comments