WAZIRI WA MAJI, NA UMWAGILIAJI MH. GERSON LWENGE AMEZIAGIZA BODI ZA MABONDE YA MAJI KUWACHUKULIA HATUA WATU WANAOFANYA KAZI KARIBU NA VYANZO VYA MAJI
TAREHE 29-09-2017
![]() |
WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI MH.GERSON LWENGE |
Waziri wa maji na umwagiliaji Mh Gerson Lwenge
ameziagiza bodi za mabonde ya maji nchini kuwachukulia hatua kali za kisheria
baadhi ya watu wanaofanya shughuli za kibinadamu karibu na vyanzo vya maji ili
kudhibiti tatizo la upotevu wa maji.
Mh Lwenge ametoa maagizo hayo wakati akizindua bodi
mpya ya bonde la ziwa Tanganyika mkoani Kigoma pamoja na ofisi mpya za mamlaka
ya bonde hilo,ambapo amesema kuwa rasilimali za maji ni lazima zisimamiwe na
bodi ili kuzua watu wanaofanya shughuli zao kandokando ya vyanzo hivyo na
kusababisha upungufu wa maji kwa wananchi.
Amesema kuwa bodi za maji zinazoanzishwa na serikali
ni muhimu sana,na lazima wajue wajibu wao kwani kuna baadhi ya wajumbe
wanaoteuliwa wakifikiri ni kwenda kupata posho pekee bila kujua kuwa wanatakiwa
kwenda kushughulikia kero za wananchi ili kuhakikisha wanapata maji safi na
salama.
Aidha waziri huyo ameongeza kuwa,hatasita kumfukuza
mwenyekiti wa bodi ya maji yeyote hapa nchini atakayeshindwa kutekeleza
majukumu yake ipasavyo ikiwemo kupeleka taarifa sahihi kwa waziri wa maji kama
sheria inavyoelekeza.
Hata hivyo ziwa la bonde Tanganyika limeelezewa
kupungua kina chake cha maji kutokana na mabadiliko ya tabia nchi na shughuli
za kibinadamu zinazofanywa na baadhi ya watu karibu na vyanzo vya maji.
WAZIRI WA MAJI, NA UMWAGILIAJI MH. GERSON LWENGE AMEZIAGIZA BODI ZA MABONDE YA MAJI KUWACHUKULIA HATUA WATU WANAOFANYA KAZI KARIBU NA VYANZO VYA MAJI
Reviewed by safina radio
on
September 29, 2017
Rating:

No comments