LIGI YA MABINGWA ULAYA YAENDELEA TENA USIKU WA KUAMKIA LEO
TAREHE 28-09-2017
Kundi A- FC Basel wakiwa
nyumbani wameibugiza Benfica 5-0, CSKA Moscow wakiwa nyumbani walikubali kipigo
cha mabao 4 -1 na Manchester United huku Romelu Lukaku akifunga mara mbili,
Martial na Mkhtaryan walifunga bao moja moja huku bao la Moscow likifungwa na
Kuachev na kuwafanya United kuongoza kundi A.
Kundi B - Psg wakiwa nyumbani
wameshinda mabao 3-0 dhidi ya Buyen Munich ambapo wachezaji Dani Alves, Neyamar
na Edison Cavanni wamefanikiwa kuifunga Bayern Munich bao 3 huku Celtic wakiwa
ugenini wakiifunga Anderchelt mabao 3 mabao ya Celtic yakiwekwa kimiani na
Patrick Roberts, Scott Sinclair na Griffiths.
Kundi C FC Qarabag imechapwa
2-1 na AS Roma, Atletico Madrid imefungwa 2-1 dhidi ya Chelsea. Kundi D-
Gonzalo Higuain na Mario Mandzukic waliisaidia Juventus kupata alama 3 baada ya
kupata ushindi dhidi ya Olympiacos wa mabao 2-0, huku Barcelona wakizidi
kujichimbia ugenini baada ya goli la kujifunga Sporting la Sebastian Coates.
LIGI YA MABINGWA ULAYA YAENDELEA TENA USIKU WA KUAMKIA LEO
Reviewed by safina radio
on
September 28, 2017
Rating:

No comments