MKUU WA MKOA WA ARUSHA BW. MRISHO GAMBO AMECHANGIA SHILINGI MILIONI MOJA NA MIFUKO HAMSINI YA SARUJI KWA AJILI YA UJENZI WA CHUMBA CHA UPASUAJI KATIKA ZAHANATI YA OLDONYOWAS MKOANI ILIYOPO ARUSHA




TAREHE 15-09-2017

MKUU WA MKOA WA ARUSHA BW. MRISHO GAMBO






Mkuu wa mkoa wa Arusha Bw Mrisho Gambo amechangia kiasi cha shilingi milioni moja pamoja na mifuko 50 ya saruji kwa ajili ya kujenga chumba cha upasuaji katika zahanati ya Oldonyowas iliyopo katika halmashauri ya wilaya ya Arusha.

Gambo amechangia fedha hizo alipokuwa akijibu  kero za wananchi wa kata hiyo za kuiomba serikali iwajengee chumba cha upasuaji kufuatia akina mama na watoto kufariki dunia pindi wanapoenda kujifungua.

Amesema kuwa kutokana na akina mama kukabiliwa na changamoto ya chumba cha upasuaji atatoa kiasi hicho cha milioni moja pamoja na mifuko 50 ili kuwezesha kunusuru maisha ya wamama wajawazito pindi wanapotaka kujifungua.

Kufuatia changamoto hiyo mkuu huyo wa mkoa amekubaliana  na wananchi wa Oldonyoas pamoja na Oldonyosambu kuchanga kila mmoja kiasi cha shilingi elfu 30 ili kuweza kujenga chumba hicho na baadaye halmashauri itamalizia ujenzi huo ambapo itakapomalizika zahanati hiyo itapanda hadhi na kuwa kituo cha afya.

Awali wakieleza kero zao kwa mkuu wa mkoa  wananchi hao wamesema kuwa katika kata hiyo wanakabiliwa na changamoto ya wamama na watoto  kupoteza maisha mara wanapofika katika zahanati hiyo kujifungua kutokana na ukosefu wa chumba cha upasuaji.

Walitaja changamoto nyingine kuwa ni pamoja na tatizo la maji,kutokuwepo kwa kituo cha polisi pamoja na mahakama na hivyo kuiomba serikali kuwasaidia kutatua changamoto hizo.
MKUU WA MKOA WA ARUSHA BW. MRISHO GAMBO AMECHANGIA SHILINGI MILIONI MOJA NA MIFUKO HAMSINI YA SARUJI KWA AJILI YA UJENZI WA CHUMBA CHA UPASUAJI KATIKA ZAHANATI YA OLDONYOWAS MKOANI ILIYOPO ARUSHA MKUU  WA  MKOA WA  ARUSHA BW. MRISHO  GAMBO AMECHANGIA SHILINGI MILIONI  MOJA  NA MIFUKO HAMSINI  YA  SARUJI  KWA  AJILI  YA UJENZI  WA CHUMBA  CHA  UPASUAJI KATIKA ZAHANATI  YA  OLDONYOWAS  MKOANI ILIYOPO  ARUSHA Reviewed by safina radio on September 15, 2017 Rating: 5

No comments