WANASAYANSI WATAKIWA KUWASAIDIA WAKULIMA WA KILIMO CHA MITI HAPA NCHINI.
TAREHE 29-09-2017
![]() |
WAZIRI WA MALI ASILI NA UTALII PRO. JUMANNE MAGHEMBE |
Waziri wa Maliasili na
Utalii Prof. Jumanne Maghembe amewataka Wanasayansi na Mashirika
yanayuojishughulisha na uhifadhi wa misitu ya ndani na nje kuwasaidia wakulima
wa kilimo cha miti kubuni mbinu mbadala wakati wakisubiri kuvuna miti yao.
Prof. Maghembe ameeleza
hayo Mkoani Morogoro katika kikao cha uimarishaji misitu na mazao ya misitu
kinachojadili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.
Kwa upande wake Mkuu wa
Mkoa,Dkt. Kebwe Stivin Kebwe ametoa wito kwa jamii kutunza Mzingira na Hifadhi
za taifa ili kujiepusha na madhara ya ukame na majangwa yanayoweza kutokea.
Kikao hicho kimeandaliwa
kwa pamoja na Muungano wa Vikundi vya Wakulima
(MVIWATA) na We Effect ya nchini Kenya na kushirikiana na mataifa kumi na saba
(17)
WANASAYANSI WATAKIWA KUWASAIDIA WAKULIMA WA KILIMO CHA MITI HAPA NCHINI.
Reviewed by safina radio
on
September 29, 2017
Rating:

No comments