MAMIA YA VIJANA WAANDAMANA KATIKA MAENEO YA UCHIMBAJI WA MADINI NCHINI GUINEA.






TAREHE 22-09-2017
VIJANA WAKIANDAMANA  NCHINI GUINEA

Mamia ya vijana wamefanya maandamano katika maeneo ya uchimbaji wa madini nchini Guinea, huku wakichoma moto kituo cha polisi pamoja na jengo lingine la umma.

Habari kutoka mji wa Kolaboui, katika wilaya ya Boke, zinasema kuwa watu kadhaa wamejeruhiwa katika makabiliano hayo kati ya walinda usalama na waandamanaji waliokuwa na marungu.

Wakaazi wa eneo hilo wanadai kutonufaika na utajiri wa madini ulio katika eneo lao.


Madini hayo ya Bauxite (Bazait) hutumika kuzalishia Alumini.
MAMIA YA VIJANA WAANDAMANA KATIKA MAENEO YA UCHIMBAJI WA MADINI NCHINI GUINEA. MAMIA   YA   VIJANA   WAANDAMANA    KATIKA  MAENEO   YA   UCHIMBAJI   WA  MADINI  NCHINI  GUINEA. Reviewed by safina radio on September 22, 2017 Rating: 5

No comments