RAIS WA MAREKANI DONALD TRUMP AMETANGAZA PUNGUZO KUBWA LA KODI


TAREHE 28-09-2017

RAIS WA MAREKANI DONALD  TRUMP

Rais Donald Trump ametangaza kile anachokiita punguzo kubwa la kodi kuwahi kutokea katika historia ya taifa hilo.

Trump amesema anahitaji mfumo rahisi na wa wazi wa kodi ili kurejesha ajira na utajiri ndani ya taifa hilo.

Trump ametangaza kupunguza kodi kwenye biashara na amesisitiza kuwa ataondoa kodi ya urithi.

Amesema kuwa wafanyakazi wanawake kwa wanaume ndiyo watakao nufaika na hatua hiyo na si wale wenye mapato makubwa na kudai kuwa mfumo wao mpya unalenga kuleta mabadiliko ambayo yatamlinda mtu wa kipato cha chini, cha kati na katika ngazi ya kaya na siyo kwa matajiri.


Hatua hii ni kutekeleza mapendekezo ya chama chake cha Republicans, huku Democrats wakiwa na maoni tofauti kwamba mabadiliko hayo yataziumiza familia zenye kipato cha kati na kupunguza kipato chao hasa wajane na watoto.
RAIS WA MAREKANI DONALD TRUMP AMETANGAZA PUNGUZO KUBWA LA KODI RAIS  WA  MAREKANI   DONALD  TRUMP  AMETANGAZA  PUNGUZO KUBWA LA KODI Reviewed by safina radio on September 28, 2017 Rating: 5

No comments