ASKARI WATATU WA ISRAEL WAMEUAWA








TAREHE 26-09-2017




Taarifa za polisi wa  Israel zinasema, askari watatu wa nchi hiyo wameuwawa katika maeneo ya Ukingo wa Magharibi,ambapo mauaji hayo yametokea baada ya Mpalestina mmoja kuwafyatulia askari hao risasi.

Mtu huyo pia alimjeruhi mmoja wa askari hao wa Israel kabla ya yeye mwenyewe kuuwawa kwa kupigwa risasi na  Mashambulio hayo yametokea wakati ambapo mjumbe wa Marekani Jason Greenblatt alikuwa mjini Jerusalem kwa mazungumzo yaliyolenga kufufua upya mpango wa amani ya Mashariki ya Kati.

Kwa mujibu wa taarifa Mpalestina huyo alifika katika lango la Har Adar pamoja na Wapalestina wengine ambao hufanya kazi za vibarua na mara moja alitoa silaha yake na kuwalenga maafisa wa polisi.

Hata hivyo Har Adat ni makaazi yaliyopo kaskazini magharibi Jerusalem karibu na Msitari wa Kijani unaotenganisha Ukanda wa Gaza na Israel.
ASKARI WATATU WA ISRAEL WAMEUAWA ASKARI   WATATU WA   ISRAEL   WAMEUAWA Reviewed by safina radio on September 26, 2017 Rating: 5

No comments