WIZARA YA MAMBO YA NJE YA MAREKANI KUTATHIMINI IWAPO ITAFUNGA UBALOZI WAKE NCHINI CUBA
TAREHE 18-09-2017
![]() |
WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA MAREKANI REX TILLERSON |
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Rex Tillerson amesema Washington inatathmini
iwapo ifunge ubalozi wake nchini Cuba, baada ya kutokea mlolongo wa
mashambulizi ya kelele kwa wafanyakazi wake.
Kwa sasa zaidi ya
wafanyakazi 20 wa ubalozi wa Marekani wameripotiwa kuwa na matatizo ya kupoteza
uwezo wa kusikia au kupatwa na mfadhaiko kutokana na sauti hiyo.
Marekani imeiambia
Cuba kuwa ina jukumu la kuwalinda wafanyakazi wote wakigeni wakiwemo Wamarekani.
Cuba imekana kuhusika
na suala hilo huku uchunguzi zaidi ukiendelea ,kujua chanzo cha watu hao
kukumbwa na matatizo hayo ya kiafya wanayoyazungumzia.
WIZARA YA MAMBO YA NJE YA MAREKANI KUTATHIMINI IWAPO ITAFUNGA UBALOZI WAKE NCHINI CUBA
Reviewed by safina radio
on
September 18, 2017
Rating:

No comments