MKUU WA MKOA WA ARUSHA BW. MRISHO GAMBO AMELIAGIZA SHIRIKA LA UMEME TANESCO KUWAPATIA UMEME WANANCHI WA MALULA WILAYANI ARUMERU MKOANI ARUSHA

TAREHE 29-09-2017
MKUU WA MKOA WA ARUSHA BW. MRISHO GAMBO

Mkuu wa mkoa wa Arusha Bw Mrisho Gambo ameliagiza shirika la umeme Tanzania TANESCO kuwapatia huduma ya umeme wananchi wa Malula na mji mdogo wa Usa river katika wilaya ya Arumeru mkoani Arusha.

Agizo hilo la mkuu wa mkoa ni utekelezaji wa agizo las rais Mh John Magufuli alilolitoa wakati akiwa njiani kuelekea uwanja wa ndege wa kimataifa wa KIA mara baada ya kuhitimisha ziara yake mkoani Arusha.

Kwa upande Mwakulishi wa meneja wa umeme hapa nchini mkoa wa Arusha Mhandisi Joanisiano Shamba amesema kuwa wananch hao watapata umeme kupitia mradi wa wakala wa nishati ya umeme vijijini REA awamu ya tatu .


Hata hivyo akiwa mkoani Arusha rais Magufuli alisimamishwa na wananchi kwa lengo la kumwelezea kero mbalimbali zinazowakabili ikiwemo tatizo la umeme,ambapo aliwataka wananchi kushirikiana na serikali ili waweze kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo. 
MKUU WA MKOA WA ARUSHA BW. MRISHO GAMBO AMELIAGIZA SHIRIKA LA UMEME TANESCO KUWAPATIA UMEME WANANCHI WA MALULA WILAYANI ARUMERU MKOANI ARUSHA MKUU   WA   MKOA   WA   ARUSHA   BW.   MRISHO  GAMBO  AMELIAGIZA    SHIRIKA   LA   UMEME  TANESCO   KUWAPATIA   UMEME   WANANCHI  WA MALULA  WILAYANI   ARUMERU   MKOANI  ARUSHA Reviewed by safina radio on September 29, 2017 Rating: 5

No comments