MADEREVA 64 WA MAGARI YA ABIRIA KUTOKA MIKOA MITATU YA KANDA YA KASKAZINI WAFUNGIWA LESENI ZAO.

TAREHE 19-09-2017



MADEREVA

Jumla ya madereva 64  wa  magari ya abiria kutoka mikoa mitatu ya kanda ya kaskazini wamefungiwa leseni zao kwa kipindi cha miezi sita baada ya kukutwa na makosa mbalimbali ya uvunjifu wa sheria za usalama barabarani.

Adhabu hiyo imetolewa na kamanda wa kikosi cha usalama wa barabarani hapa nchini SACP Fortunatus Musilimu wakati wa operesheni maalumu aliyoifanya ya kubaini madereva wanaokiuka sheria za usalama wa barabarani katika mikoa ya Arusha,Kilimanjaro na Manyara.

Kamanda Musilimu amesema kuwa kati ya madereva hao 47 ni kutoka mkoa wa Kilimanjaro,13 kutoka mkoa wa Arusha na 4 wa mkoa wa Manyara ambao watatumikia adhabu hiyo kw akipindi cha miezi na baada ya muda huo kwisha madereva hao watatainiwa upya ili kuona kama wanafaa kurudishiwa leseni zao.


Amesema kuwa moja ya makosa hayo ni kuendesha kwa mwendo kasi hali inayohatarisha maisha ya abiria,ambapo amesema kuwa operesheni hiyo itakuwa endelevu lengo likiwa ni kupunguza ajali zitokanazo na uzembe na kupoteza nguvu kazi ya taifa.
MADEREVA 64 WA MAGARI YA ABIRIA KUTOKA MIKOA MITATU YA KANDA YA KASKAZINI WAFUNGIWA LESENI ZAO. MADEREVA   64   WA  MAGARI  YA   ABIRIA  KUTOKA   MIKOA  MITATU  YA  KANDA  YA  KASKAZINI  WAFUNGIWA    LESENI   ZAO. Reviewed by safina radio on September 19, 2017 Rating: 5

No comments