Waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Mh Ummy Mwalimu amewataka waganga wakuu wa mikoa na wilaya hapa nchini kuwachukulia hatua za kisheria watu wote wanaouza madawa ya tiba asili kinyume na sheria.
TAREHE 6 SEPTEMBER 2017
![]() |
WAZIRI
WA AFYA WAZEE JINSIA NA WATOTO MH UMMY MWALIMU
|
Waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Mh Ummy Mwalimu amewataka waganga wakuu wa mikoa na wilaya hapa nchini kuwachukulia hatua za kisheria watu wote wanaouza madawa ya tiba asili kinyume na sheria.
Mh Mwalimu
ameyasema hayo leo bungeni mjini Dodoma wakati akijibu swali la mbunge wa Konde
Mh Khatibu Haji aliyetaka kujua ni utaratibu gani unaotumiwa na serikali katika
kuwaruhusu watu mbalimbali kuuza madawa ya tiba asili kutokana na matangazo
mengi yanayobandikwa mitaani na kusababisha usumbufu mkubwa kwa wananchi.
Amesema kuwa
ili mtu aruhusiwe kuuza madawa ya tiba asili ni lazima asajiliwe kwenye baraza
la tiba asili na tiba mbadala baada ya kudhibitishwa na mkemia mkuu wa serikali
pamoja na mamlaka ya chakula na dawa TFDA kama hazina madhara kwa binadamu
hivyo mtu yeyote anayefanya biashara hiyo bila kusajiliwa anavunja sheria hivyo
anatakiwa kukamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria.
Mh waziri
amesema utaratibu wa usajili upo kwa mujibu wa sheria ya nchi ya mwaka wa 2002
na kanuni zake,ambapo pia amewataka wananchi kufanya mazoezi ili kuepukana na
matatizo mbalimbali yanayowafanya kukimbilia kununua dawa hizo ikiwemo upungufu
wa nguvu za kiume.
Hata hivyo
bunge la kumi na moja mkutano wa nane unaendelea mjini Dodoma ambapo wabunge
watajadili miswada mbalimbali ya kisheria na mkutano huo unatarajiwa
kuhitimishwa Sept 15 mwaka huu.
Waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Mh Ummy Mwalimu amewataka waganga wakuu wa mikoa na wilaya hapa nchini kuwachukulia hatua za kisheria watu wote wanaouza madawa ya tiba asili kinyume na sheria.
Reviewed by safina radio
on
September 06, 2017
Rating:

No comments