WAZIRI WA UJENZI NA MAWASILIANO MH. MAKAME MBARAWA MNYAA AWATAKA WADAU WA MAWASILIANO YA ANGA KUTATUA CHANGAMOTO ZILIZOPO KATIKA SEKTA HIYO.



TAREHE  20-09-2017
WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI  NA MAWASILIANO  MH.  MAKAME   MBARAWA   MNYAA


Waziri wa ujenzi uchukuzi na mawasiliano Mh Makame Mbarawa Mnyaa amewataka wadau wa mawasiliano ya anga hapa nchini kutatua changamoto zilizopo katika sekta hiyo ili kuwezesha uchumi wa Tanzania ya viwanda.

Mh Mnyaa ametoa kauli hiyo wakati akizungumza katika kongamano la kwanza la mamlaka ya usafiri wa anga jijini Dar-es-salaam,ambapo amesema kuwa serikali iko tayari kushirikiana na wadau wa mamlaka ya anga katika kukabiliana na changamoto zinazokabili mamlaka hiyo ikiwemo upungufu wa wataalamu.

Amesema kuwa serikali imeamua kukutana na wadau hao ili kujadiliana namna ya kumaliza changamoto hizo zinazoikabili sekta ya anga ikiwemo usafirishaji wa bidhaa mbalimbali kupitia viwanja vya ndege vya nje badala ya viwanja vya ndani hali inayosababisha Tanzania kupoteza mapato mengi ambayo yangeweza kuinua uchumi wa Taifa.

Kwa upande wake mkurungenzi mkuu wa mamlaka ya usafiri wa anga nchini TCAA Bw Hamza Johari amewataka wanafunzi kusoma masomo ya sayansi ili Tanzania iweze kuwa na wataalamu wenngi zaidi hasa katika sekta ya anga ambayo ina upungufu mkubwa wa wataalamu.


Hata hivyo mamlaka ya anga hapa nchini ina wataalamu 20 pekee huku mahitaji halisi ya wataalamu wanaotakiwa ikiwa ni 50.
WAZIRI WA UJENZI NA MAWASILIANO MH. MAKAME MBARAWA MNYAA AWATAKA WADAU WA MAWASILIANO YA ANGA KUTATUA CHANGAMOTO ZILIZOPO KATIKA SEKTA HIYO. WAZIRI  WA  UJENZI  NA  MAWASILIANO  MH. MAKAME  MBARAWA  MNYAA   AWATAKA  WADAU  WA  MAWASILIANO   YA  ANGA   KUTATUA   CHANGAMOTO  ZILIZOPO  KATIKA   SEKTA HIYO. Reviewed by safina radio on September 20, 2017 Rating: 5

No comments