MAMLAKA ZA UPIMAJI MAENEO MKOANI DODOMA ZIMEAGIZWA KUTOA VIWANJA KWA GHARAMA NAFUU

TAREHE 28-09-2017


Mamlaka zinazohusika na upimaji wa maeneo  mkoani Dodoma zimeagizwa kuzipatia viwanja kwa gharama nafuu taasisi zinazotaka kujenga ofisi na makazi mkoani humo ili kuunga mkono mpango wa serikali wa kuhamia Dodoma.

Agizo hilo limetolewa na mkuu wa mkoa wa Dodoma Bw Jordan Rwigimbana wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya miradi mbalimbali ya ujenzi inayoendelea mkoani humo.

Katika ziara hiyo mkuu huyo wa mkoa amepokea malalamiko kutoka kwa baadhi ya taasisi za kukwamisha ujenzi na kutotoa ushirikiano hali iliyomlazimu kuzitaka mamlaka husika kuzipatia taasisi hizo maeneo kwa gharama nafuu ili nyumba zinazojengwa zikamilike kwa wakati.


Hata hivyo mji wa Dodoma unaendelea kujengwa baada ya serikali ya awamu ya tano kuamua kuhamishia shughuli zake mkoani humo ambako ndiko makao makuu ya nchi.
MAMLAKA ZA UPIMAJI MAENEO MKOANI DODOMA ZIMEAGIZWA KUTOA VIWANJA KWA GHARAMA NAFUU MAMLAKA  ZA  UPIMAJI  MAENEO  MKOANI   DODOMA   ZIMEAGIZWA  KUTOA  VIWANJA  KWA  GHARAMA  NAFUU Reviewed by safina radio on September 28, 2017 Rating: 5

No comments