SANCHEZ AINGOZA ARSENAL KATIKA USHINDI WA 3-1 DHIDI YA FC COLOGNE YA UJERUMANI KATIKA MICHUANO YA EUROPA LIGI
TAREHE 15-09-2017
![]() |
MCHEZAJI WA ARSENAL ALEXIS SANCHEZ |
Alexis
Sanchez aliisaidia Arsenal kutoka nyuma na kupata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya
klabu ya Ujerumani Cologne katika mechi ya Yuropa iliocheleweshwa kwa saa moja
kutokana na matatizo ya mashabiki.
Sanchez ambaye karibia aihame klabu hiyo
ili kujiiunga na Manchester City katika siku ya mwisho ya uhamisho , aliuchukua
mpira nje ya eneo hatari na kuupinda huku kipa Timo akishindwa kuokoa mkwaju
huo.
Mechi hiyo hatahivyo
haikuanza katika muda iliopangiwa baada ya maelfu ya mashabiki wa Cologne
kuwasili katika uwanja wa Emirates bila tiketi na baadaye kuzozana na
wanaowakaribisha wageni ndani ya uwanja huo.
Na mechi ilipoanza , Cologne
ilichukua uongozi baada ya Jhon Cordoba kumfunga kipa David Ospina akiwa maguu
40.
Mshambuliaji Olivier Giroud alipiga nje
kichwa cha wazi akiwa maguu sita pekee karibu na goli .
Lakini mchezaji wa ziada Sead
Kolasinac alisawazisha kabla ya Sanchez kufunga bao la pili.
Beki wa kulia wa Arsenal
Hector baadaye alifunga bao la tatu huku kiungo wa kati wa Arsenal Jack
Wilshere akiichezea klabu hiyo kwa mara ya kwanza tangu Agosti 2016.
Katika
mchezo mwingine Everton wameanza vibaya michuano ya Europa baada ya kufungwa
bao 3 kwa nunge na Atlanta, huku Villareal wakiipiga Fc Astana bao 3 kwa 1.
Andre Silva
aliifungia Ac Millan hattrick wakati wakiichapa Austria Vienna bao 5 kwa 1,
huku Suso na Calhanoglu wakiipatia Ac Millan mabao mengine na lile la Austria
Vienna likiwekwa kimiani na Borkavic.
SANCHEZ AINGOZA ARSENAL KATIKA USHINDI WA 3-1 DHIDI YA FC COLOGNE YA UJERUMANI KATIKA MICHUANO YA EUROPA LIGI
Reviewed by safina radio
on
September 15, 2017
Rating:

No comments