MKUTANO WA SABA WA BARAZA LA WAWAKILISHI KUANZA KESHO JUMATANO

TAREHE 26-092017


Mkutano wa saba wa baraza la tisa la wawakilishi unatarajiwa kuanza Jumatanao wiki hii ambapo patakuwepo na shughuli mabalimbali ikiwemo kipindi cha maswali na majibu ambapo jumla ya maswali mia moja thelethini na saba yatajibiwa.

Akitoa taarifa ya kuanza kwa mkutano huo mbele ya waandishi wa habari mjini Unguja katibu wa baraza la wawakilishi Raya Issa amesema kuw apamoja na mambo mengine muswada ya sheria ambayo iliwasilishwa na kusomwa katika mkutano uliopita itasomwa na kujadiliwa tena katika vikao hivyo vya wawakilishi.

Katibu huyo ametaja miswada itakayojadiliwa kuwa ni pamoja na mswada wa kufuta sheria namba tatu ya mahakama ya kadhi ya mwaka wa 1985 na mswada wa sheria ya kuanzisha baraza la taifa la biashara.


Hata hivyo mkutano huo pia unatarajia kujadili ripoti za wizara za serikali ya mapinduzi ya Zanzibar kuhusu utekelezaji wa maagizo ya kamati za baraza hilo ikiwemo ripoti ya utekelezaji wa mamlaka ya maji Zanzibar ZAWA.
MKUTANO WA SABA WA BARAZA LA WAWAKILISHI KUANZA KESHO JUMATANO MKUTANO  WA  SABA  WA  BARAZA  LA  WAWAKILISHI  KUANZA KESHO JUMATANO Reviewed by safina radio on September 26, 2017 Rating: 5

No comments