WATU ZAIDI YA 140 WAFARIKI DUNIA KATIKA TETEMEKO LA ARDHI NCHINI MEXICO
TAREHE 20-09 -2017
![]() |
MIILI YA WATU WALIOFARIKI DUNIA |
Tetemekokubwa la ardhi limekumba
maeneo ya katikati mwa Mexico na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 140 huku
jitihada za uokozi zikiendelea.
Tetemeko lenye nguvu ya kipimo cha
saba nukta moja kwa vipimo vya Richter limedondosha karibu majengo 30 katika
mji mkuu wa Mexico city.
Watu wanaotoa huduma za dharura
wakisaidiwa na mamia ya watu wanaojitolea bado wanaendelea kutafuta manusura
ambao wamefukiwa na kifusi.
Maafisa wa serikali nchini wanasema
idadi ya waliokufa inaweza kuongezeka ambapo mwandishi wa habari aliyekuwa
mjini Mexco city Bi Natasha Pizzey amesema kuwa kuna idadi kubwa ya watu
waliofukiwa na kifusi baada ya majengo kuporomoka.
Mapema mwezi huu tetemeko hilo la
ardhi pia lilipita katika eneo la pwani ya kusini magharibi mwa Mexico na
kusababisha vifo vya watu 90.
WATU ZAIDI YA 140 WAFARIKI DUNIA KATIKA TETEMEKO LA ARDHI NCHINI MEXICO
Reviewed by safina radio
on
September 20, 2017
Rating:

No comments