SERIKALI YA TANZANIA KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA SERKALI YA MAPINDIZI YA ZANZIBAR KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA.


Naibu waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu sera,bunge,ajira,vijana na watu wenye ulemavu Mh Antony Mavunde amesema kuwa serikali ya Tanzania itaendelea kushirikiana na serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kupambana na biashara haramu ya madawa ya kulevya.

Image result for PICHA YA ANTONY MAVUNDE
MH.MAVUNDE
Mh Mavunde ameyasema leo bungeni mjini Dodoma wakati akijibu swali la mbunge wa viti maalumu kutoka Zanzibar Mh Asha Abdalah aliyetaka kujua serikali ina mpango gani wa kupambana na wafanya biashara wa madawa ya kulevya wanaotumia viwanja vya ndege vya Zanzibar kusafirisha madawa hayo.

Amesema kuwa baada ya Tanzania bara kuanza kupambana na watumiaji na wafanyabiashara hao kwa kuziba mianya ya kusafirisha madawa hayo kupitia viwanja vyake vya ndege wafanyabiashara hao walihamia Zanzibar hivyo ili kupambana na hali hiyo wameamua kushirikiana kupambana na wahusika wote wanaohusika na biashara hiyo haramu.

Katika hatua nyingine naibu waziri Mavunde amesema kuwa serikali ina mpango wa kuanzisha madirisha ya kuwahudumia waathirika wa matumizi ya madawa ya kulevya katika hospitali za mikoa lengo likiwa ni kuwasaidia kuwapa matibabu waathirika hao kwa ukaribu zaidi.

Hata hivyo bunge la 11 mkutano wa 11 umenza leo bungeni mjini Dodoma mkutano ambao utakuwa ni maalumu kwa ajili ya kujadili na kupitisha bajeti ya mwaka wa fedha wa 2018/2019.

SERIKALI YA TANZANIA KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA SERKALI YA MAPINDIZI YA ZANZIBAR KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA. SERIKALI YA TANZANIA KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA SERKALI YA MAPINDIZI YA ZANZIBAR KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA. Reviewed by safina radio on April 03, 2018 Rating: 5

No comments