ISRAEL YAFIKIA MAKUBALIANO NA UMOJA MATAIFA.
Serikali ya Israel
imesema imefikia makubaliano na Umoja wa Mataifa ya kuwapeleka katika nchi za
Magharibi kiasi ya Waafrika elfu kumi na sita wanaoomba hifadhi.
NETANYAHU |
Mpango huo wa Shirika
la Umoja wa Mataifa la Kuwahudumia Wakimbizi, UNHCR, utafanikisha kuwapeleka
kiasi ya wahamiaji zaidi ya elfu 16 kati ya elfu thelathini na saba kwenye nchi
za Ujerumani, Canada na Italia.
Hata hivyo, mawaziri
kadhaa wa Israel wameupinga mpango huo, wakisema kuwa Waziri Mkuu Benjamin
Netanyahu, hakuwaarifu kabla kuhusu makubaliano hayo.
Ujerumani na Italia pia zimeelezea wasiwasi
wao kuhusu mpango huo baada ya kila mmoja kusema hawakufahamishwa kuhusu hilo.
Ofisi ya Netanyahu
imesema mpango huo utachukua nafasi ya mpango uliowekwa awali wa kuwarejesha
wahamiaji kwenye nchi ya Afrika ambayo ilikuwa haijatajwa.
ISRAEL YAFIKIA MAKUBALIANO NA UMOJA MATAIFA.
Reviewed by safina radio
on
April 03, 2018
Rating:
No comments