SHIRIKA LA ECHO KUENDELEA KUPIGA VITA GUGU KAROTI


Shirika la lisilokuwa la kiserikali la ECHO linalofanya kazi na wakulima na wafugaji limefanikiwa kutoa elimu ya kuthibiti gugu karoti kwa shule za msingi na sekondari za jiji la Arusha kwa lengo la kuwaepusha na madhara yatokanayo na majani hayo.
Image result for PICHA YA GUGU KAROTI
PICHA YA GUGU KAROTI

Hayo yameelezwa na Afisa Maendeleo ya Jamii wa Shirika la ECHO nchini Malvery Begry, wakati akizungumza na waandishi wa habari jinsi ambavyo wamekuwa wakielimisha jamii na shule mbali mbali namna ya kudhibiti jani hilo.

Bw. Begry, amesema kuwa kutokana na majani hayo aina ya gugu karoti kuwa na madhara kwa wakulima na wafugaji na hata wanafunzi mashuleni wameweza kutoa elimu kuhusiana na jani hilo ili waweze kuepuka athari za majani hayo.

Aidha, amesema kuwa mbali na kutoa elimu hiyo wamekuwa wakishirikiana kwa pamoja na viongozi wa vijiji kung’oa majani hayo ambayo yamekuwa yakiathiri afya za wananchi pamoja na mifugo.

Kwa upande wake Bw Shamba wa Shirika hilo Charles Bonivencha amesema kuwa kutokana na majani hayo kuwa na madhara ya kiafya kwa binadamu wamekuwa wakihamasisha jamii kuhakikisha wanang’oa majani hayo na kuyachoma ili waweze kulitokomeza.

SHIRIKA LA ECHO KUENDELEA KUPIGA VITA GUGU KAROTI SHIRIKA LA ECHO KUENDELEA KUPIGA VITA GUGU KAROTI Reviewed by safina radio on April 03, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.