SERIKALI YA LIBYA YAANZA OPERESHENI YA MASHAMBULIO DHIDI YA DAESH.


Serikali ya umoja wa kitaifa ya Libya imetangaza kuwa jeshi lake limeanza kutekeleza operesheni ya mashambulio dhidi ya kundi la kigaidi la DAESH magharibi mwa nchi hiyo.
Image result for PICHA YA ASKARI WA KUNDI LA DAESH
Kupitia taarifa iliyotoa hapo jana, serikali ya umoja wa kitaifa ya Libya imetangaza kuwa jeshi la nchi hiyo limeanza kutekeleza operesheni ya kijeshi ya kuwasaka wanachama wa Daesh ambao wangali wanaendesha harakati zao magharibi mwa nchi.
Muhammad As-Salik,ambaye ni msemaji wa Waziri Mkuu wa serikali ya umoja wa kitaifa ya Libya Fayez al-Sarraj amesema, miongoni mwa malengo ya operesheni hiyo ya kijeshi ni kuvilenga vituo na ngome zote za kigaidi kandokando ya mji wa Misrata ulioko kilomita 200 mashariki mwa mji mkuu Tripoli.
Libya imekuwa ikishuhudia ongezeko la harakati za makundi ya kigaidi,  na hali ya mchafuko pamoja na matatizo ya kisiasa na kiuchumi tangu yalipojiri mabadiliko ya kisiasa mwaka 2011 na kuvurugika uthabiti uliosababishwa na uingiliaji kijeshi wa Marekani na shirika la kijeshi la NATO.

SERIKALI YA LIBYA YAANZA OPERESHENI YA MASHAMBULIO DHIDI YA DAESH. SERIKALI YA LIBYA YAANZA OPERESHENI YA MASHAMBULIO DHIDI YA DAESH. Reviewed by safina radio on April 03, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.