MAFURIKO YAWAACHA WATU BILA MAKAZI NA KUHARIBU EKARI 50 ZA MAZAO YA CHAKULA, ARUSHA.


Zaidi  ya  kaya  kumi (10)  zimeachwa  bila  makazi  kufuatia mafuriko  ya  mvua  zilizonyesha usiku  wa  kuamkia  leo   katika  kata  ya Bwawani  wilayani  Arumeru mkoani  Arusha ikiwa  ni  pamoja  na  uharibifu  wa takribani ekari 50 za  mazao  ya  chakula. 

Image result for mafuriko
Wananchi waachwa bila makazi kutokana na mafuriko.
Akizungumzia maafa hayo ndugu Jeremia  Kisiongo  mollel mwenyekiti wa  kitongoji  cha  darajani kijiji  cha  kigongoni amesema kuwa mazao ya chakula  yaliyoharibiwa na mvua ni mahindi pamoja na  maharage sambamba na miundombinu ya  barabara.

Aidha wakati akiambatana na Msafara wa wasamaria wema mwenyekiti  huyo   umeshuhudia  baadhi  ya  familia  zikilazimika  kuhamisha  familia  zao  kwenda  kuwatafutia hifadhi  kwa  ndugu   na  jamaa walioko  kata za  jirani  huku  wengine  wakiwa  wanatumia  ndoo , plastiki  na  sufuria kusomba  maji  yaliyojaa  ndani  ya  nyumba  zao huku mifugo ikikosa hifadhi.

Kufuatia  hali  hiyo  Bw kisiongo  ametumia  fursa  hiyo kuomba  msaada kwa  wasamaria wema,serikali ya wilaya pamoja na  mkoa  wa  Arusha  kutembelea eneo  hilo ili  kujionea  kiwango cha madhara  yaliyosababishwa  na  mvua  hizo na kuwasaidia wahanga wa mvua hizo kusudi wasipatwe na madhara yatokanayo  na  mafuriko  ya  mvua.

Akizungumza na redio safina mmoja  kati  wanaharakati wafuatiliaji  kiwango  cha  uharibifu  wa  mvua  katika maeneo  hayo  ndugu  Frenki  Lobulu  Mollel amesema kuwa leo majira ya  jioni  baadhi  ya familia  zilizokosa  makazi ni  pamoja  na nyumba  za  boma  la   Kiroroma  na   nyumba  za  Boma  la  Namoyo  katika  eneo  la  kitongojini katika kata hiyo .

MAFURIKO YAWAACHA WATU BILA MAKAZI NA KUHARIBU EKARI 50 ZA MAZAO YA CHAKULA, ARUSHA. MAFURIKO YAWAACHA WATU BILA MAKAZI NA KUHARIBU EKARI 50 ZA MAZAO YA CHAKULA, ARUSHA. Reviewed by safina radio on April 03, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.