WATU MIA MOJA WAMEUAWA NCHINI AFGHANISTAN.

Zaidi ya watu 100,  wameuawa na wengine kujeruhiwa jana Jumatatu katika shambulizi la bomu lililotekelezwa na ndege ya jeshi la Afghanistan.

Image result for MAUAJI AFGHANISTAN.
Shamulizi la bomu Afughanstan.

Kulingana na ripoti kutoka hospitali na vyanzo vya usalama Shambulio hilo lilitokea katika chuo cha dini (madrasa) kaskazini mashariki mwa Afghanistan
Shambulio hilo lilitokea Jumatatu mchana wakati wa sherehe ya kuhitimu visomo mwaka katika chuo hicho cha dini (madrasa), katika wilaya inayodhibitiwa kwa kiasi kikubwa na kundi la Taliban.
Msemaji wa Wizara ya Afya mjini Kabul, Wahid Majroh, amethibitisha leo Jumanne asubuhi kuwa watu 57, ikiwa ni pamoja na watoto na wazee, walisafirishwa hospitalini katika mkoa wa Kunduz na watano waliopoteza maisha.

WATU MIA MOJA WAMEUAWA NCHINI AFGHANISTAN. WATU MIA MOJA WAMEUAWA NCHINI AFGHANISTAN. Reviewed by safina radio on April 03, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.