RAIS WA UTURUKI KUKUTANA NA RAIS WA URUSI NA IRAN.
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan anatazamia kuwapokea leo
Jumatano marais wenzake washirika wawili muhimu wa Syria kutoka Irani, Hassan
Rohani, na Urusi, Vladimir Putin,.
ERDOGAN RAIS WA UTURUKI. |
Taarifa zinaeleza kuwa Viongozi hao watajadili mustakabali wa
Syria iliyoharibiwa na vita kwa muda wa miaka saba.
Viongozi hao watatu ni washirika muhimu wa rais wa Syria Bashar
Al Assad ambapo Mkutano huo ni
uendelezaji wa mchakato wa Astana, ambao haujumuishi Washington na unakinzana
na mazungumzo ya Umoja wa Mataifa.
Mchakato huu, uliozinduliwa na nchi hizi tatu mnamo mwezi
Januari 2017, ulipelekea kufikiwa makubaliano kuhusu kutengwa kwa maeneo manne
yanayokabiliwa na vita nchini Syria.
Hata hivyo suala la
kutafuta suluhu ya mgogoro wa Syria, ambapo upinzani wa Syria umeendelea
kugawanyika na kuwa dhaifu, limeendelea kuzua tofauti ya maslahi kati ya
Moscow, Ankara na Tehran.
RAIS WA UTURUKI KUKUTANA NA RAIS WA URUSI NA IRAN.
Reviewed by safina radio
on
April 04, 2018
Rating:
No comments