SAAD GADAFFI AFUTIWA MASHITAKA.
Mahakama ya Tripoli imefuta kesi ya mauaji iliyokua ikimkabili
Saadi Gaddafi, mtoto wa tatu wa aliyekua rais wa Libya, Muammar Gaddafi.
Saadi Gaddafi amefutiwa mashtaka yote dhidi yake katika kesi ya
mwanamichezo Bachir al-Rayani ambaye alifariki dunia mnamo mwaka 2006 baada ya
kupigwa kichwani.
SAAD GADAFFI. |
Bachir Rayani alifariki dunia baada ya malumbano katika nyumba
inayomilikiwa na Saadi Gaddafi.
Tangu mwanzoni mwa mwaka huu, mahakama imerejelea hukumu za
maafisa wa zamani wa Libya baada ya kuhamishwa kutoka gereza la al-Hadaba
kwenda sehemu iliyo chini ya usimamizi wa Wizara ya Sheria.
Kwa mujibu wa waangalizi kadhaa, uamuzi huu unaonekana kuwa ni
utabiri wa kukabiliana na kesi nyingine za wakuu wa serikali ya zamani ya
Libya, ambao wamekuwa wakisubiri haki kwa miaka kadhaa.
Hata hivyo Familia ya Bachir al-Rayani, imepinga uamuzi huo na
kuelezea masikitiko yake kwa maelezo kuwa wana ushahidi wa Saadi Gaddafi kuhusika katika kifo
hicho.
SAAD GADAFFI AFUTIWA MASHITAKA.
Reviewed by safina radio
on
April 04, 2018
Rating:
No comments