SERIKALI YA CONGO YASEMA MONUSCO INAPASWA KUONDOKA NCHINI HUMO IFIKAPO 2020.


Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo inataka kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Mataifa nchini Kongo, MONUSCO kuondoka nchini humo ifikapo mwaka 2020.
Image result for monusco DRC
Jeshi la Umoja wa Mataifa la Kuleta Amani-MONUSCO nchini DRC.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Kongo, Leonard She Okitundu amesema hayo baada ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wiki iliyopita kupiga kura ya kuongeza mamlaka ya kikosi hicho kwa mwaka mmoja zaidi.
She Okitundu amewaambia waandishi habari mjini Kinshasa kuwa wamelijulisha baraza hilo kwamba mamlaka ya sasa ndiyo ya mwisho, kabla ya kikosi hicho hakijaondoka Kongo baada ya kuwepo nchini humo kwa miaka 20.
Umoja wa Mataifa umeonya kuhusu kuongezeka kwa mzozo wa kibinaadamu nchini Kongo, huku kiasi ya Wakongo milioni 13.1 wakiwa wanahitaji msaada.
Hata hivyo Waziri huyo amethibitisha kuwa Kongo haitohudhuria mkutano wa wafadhili ulioandaliwa na Umoja wa Mataifa na Umoja wa Ulaya ambao umepangwa kufanyika Geneva Aprili 13.

SERIKALI YA CONGO YASEMA MONUSCO INAPASWA KUONDOKA NCHINI HUMO IFIKAPO 2020. SERIKALI YA CONGO YASEMA MONUSCO INAPASWA KUONDOKA NCHINI HUMO IFIKAPO 2020. Reviewed by safina radio on April 04, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.