MUHAGAMA AWATAKA VIJANA KUJIUNGA KATIKA VIKUNDI ILI KUFAIDI ASILIMIA TANO YA FEDHA ZA SERIKALI.


Waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu sera bunge ajira vijana na watu wenye ulemavu Mh Jeenister Mhagama amewataka vijana hapa nchni kujiunga kwenye vikundi mbalimbali vya SACCOS katika maeneo yao ili waweze kufaidika na fedha za asilimia tano zinatolewa na serikali katika kila halmashauri.

Image result for MH. JENISTA MHAGAMA BUNGENI DODOMA.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge Ajira Vijana na Watu Wenye Ulemavu Mh Jeenister Mhagama 
Mh Mhagama ameyasema hayo leo bungeni mjini Dodoma wakati akijibu swali la nyongeza la mbunge wa viti maalumu kutoka mkoa wa kigoma Mh Josephine Gezebuke aliyetaka kujua vijana wanapataje asilimia tano za fedha zinazotengwa na halmashauri zao kama ilivyoagizwa na serikali .

Amesema kuwa njia rahisi ya vijana kukopeshwa fedha hizo ni kujiunga na SACCOS zilizoanzishwa katika halmashauri zao na hiyo itasaidia vijana kuanzisha shughuli mbalimbali za ujasiriamali kwa ushirikiano kuliko  kumkopesha kijana mmoja mmoja.

Ameongeza kuwa fedha ambazo ni asilimia tano kwa vijana na asilimia tano kwa wanawake hutengwa na halmashauri kwa ajili ya kusaidia makundi hayo kujikwamua na umaskini.

Hata hivyo mkutano wa 11 bunge la 11 linaendelea mjini Dodoma likiwa ni maalumu kwa ajili ya kujadili na kupitisha bajeti katika mwaka wa fedha wa 2018/2019.

MUHAGAMA AWATAKA VIJANA KUJIUNGA KATIKA VIKUNDI ILI KUFAIDI ASILIMIA TANO YA FEDHA ZA SERIKALI. MUHAGAMA AWATAKA VIJANA KUJIUNGA KATIKA VIKUNDI ILI KUFAIDI ASILIMIA TANO YA FEDHA ZA SERIKALI. Reviewed by safina radio on April 04, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.