SHINYANGA NA TABORA ZALENGA KUNUSURU MIKOA HIYO KUGEUKA KUWA JANGWA KWA UPANDAJI MITI.
Mikoa ya Shinyanga na Tabora imetangaza kuanza
mpango maalumu wa kugawa miche ya miti kila kaya iliyokabiliana na ukame katika
mikoa hiyo.
Miche ya Miti. |
Wakizungumza mara baada ya zoezi la upandaji miti Wilayani
Kishapu Mkoani Shinyanga Wakuu wa Mikoa hiyo Zainabu Telack wa Shinyanga na Agrey
Mwanri wa Tabora wamesema kuwa hatua hiyo inalenga kunusuru mikoa hiyo kugeuka
kuwa jangwa.
Aidha, Wakuu hao wamekutana katika kijiji cha
Mwatuju ikiwa ni hatua ya kunusuru ukame katika mikoa hiyo wakati wa kuelekea
kilele cha maadhimisho ya siku ya upandaji miti kitaifa yanayotarajiwa
kufanyika tarehe tano mwezi huu Wilayani Kishapu mkoani Shinyanga.
Hata hivyo Kauli mbiu ya maadhimisho ya upandaji
miti kitaifa ni Tanzania ya viwanda inawezekana, panda miti kwa maendeleo ya
viwanda.
SHINYANGA NA TABORA ZALENGA KUNUSURU MIKOA HIYO KUGEUKA KUWA JANGWA KWA UPANDAJI MITI.
Reviewed by safina radio
on
April 04, 2018
Rating:
No comments