ZAIDI YA WAKAZI 2000 WATAFAIDIKA NA HUDUMA ZA TANESCO BAADA YA KUFUNGULIWA KWA OFISI ZAKE.
Zaidi ya wakazi elfu mbili wa kata ya Madibira
Wilayani Mbarali Mkoani Mbeya wataondokana na adha ya kutembea umbali mrefu wa
zaidi ya kilometa themanini kutafuta huduma za TANESCO kutokana na Shirika hilo kufungua
ofisi sehemu ya karibu inayowawezesha wananchi wote kupatiwa huduma kwa ukaribu.
Naye, Meneja wa TANESCO mkoa wa Mbeya Mhandisi
Benedikti Bahati amesema kuwa shirika hilo litaendelea kusogeza huduma kwa
wananchi hasa maeneo ya vijijini.
Kwa upande wa baadhi ya wananchi hao wamesema kuwa baada ya
kufunguliwa ofisi hizo za TANESCO katika eneo hilo kunaleta matumaini mapya ya
kuwa na uhakika wa huduma tofauti na ilivyokuwa hapo awali.
Hata hivyo, wananchi hao wamesema kuwa awali
walikuwa wakifuata huduma za TANESCO mjini Lujewa jambo lililokuwa linasababisha
maendeleo yao kurudi nyuma.
ZAIDI YA WAKAZI 2000 WATAFAIDIKA NA HUDUMA ZA TANESCO BAADA YA KUFUNGULIWA KWA OFISI ZAKE.
Reviewed by safina radio
on
April 04, 2018
Rating:
No comments