RAIS MAGUFULI KUWA MGENI RASMI KATIKA UZINDUZI WA NYUMBA ZA POLISI.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa nyumba za polisi utakaofanyika tarehe 7 mwezi huu katika uwanja wa mpira wa Sheikh Amri Abeid Mkoani Arusha.

Image result for PICHA YA RAIS MAGUFULI
RAIS MAGUFULI

Akitoa taarifa hiyo kwa waandishi wa habari Kamanda wa polisi Mkoa wa Arusha Naibu Kamishna wa polisi DCP Charles Mkumbo amesema kuwa uzinduzi huo utaenda sambamba na maonesho mbalimbali ya jinsi jeshi la polisi linavyofanya kazi za kuhudumia wananchi.

Vilevile Kamanda Mkumbo amesema kuwa sambamba na uzinduzi huo pia Mh.Rais ataongoza zoezi la ufunguzi wa vituo viwili vya polisi kikiwemo kituo cha utalii na diplomasia ambacho ni cha kwanza kujengwa nchini pamoja na kituo cha kisasa cha daraja la kati ambacho kitatoa huduma katika Kata ya Muriet Mkoani hapa.

Kamanda Mkumbo ametoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi katika kushuhudia maonesho hayo ambapo amesema tukio hilo halitoathiri kufanyika kwa shughuli nyingine za kijamii hususan huduma za barabarani. 

Hata hivyo uzinduzi wa nyumba hizo unafanyika kutokana na kujengwa kwa nyumba mpya za jeshi la polisi  baada ya  kuungua kwa nyumba za awali za askari polisi mnamo tarehe 27 mwezi wa 9 mwaka jana,janga ambalo lilisababisha kuteketea kwa mali zote za askari hao.

RAIS MAGUFULI KUWA MGENI RASMI KATIKA UZINDUZI WA NYUMBA ZA POLISI. RAIS MAGUFULI KUWA MGENI RASMI KATIKA UZINDUZI WA NYUMBA ZA POLISI. Reviewed by safina radio on April 05, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.