WAZIRI NCHEMBA AWAOMBA VIONGOZI WA DINI KUWAELIMISHA WAUMINI WAO ILI WAEPUKANE NA UNYANYASAJI.
Waziri wa mambo ya ndani ya nchi Mh Mwigulu Nchemba
amewaomba viongozi wa dini hapa nchini kuwaelimisha waumini wao ili waweze
kuepukana na unyanyasaji wa kijinsia unaofanywa na baadhi ya watu hapa nchini.
WAZIRI NCHEMBA |
Mh Nchemba ameyasema hayo leo bungeni mjini Dodoma
wakati akijibu maswali ya wabunge bungeni ambapo amesema kuwa unyanyasaji wa kijinsia wanaofanyiwa wanawake
na watoto unatokana na watu kutokuwa na hofu ya Mungu hivyo endapo viongozi wa
dini watatoa elimu hiyo vitendo hivyo vitapungua kwa kiasi kikubwa.
Amesema kuwa ili kukabiliana na hali hiyo serikali
imeweka madawati ya kijinsia katika vituo mbalimbali vya polisi hapa nchini
hivyo ni vyema watu wanaofanyiwa ukatili huo wakaripoti katika vituo hivyo ili
wahusika waweze kuchukuliwa hatua za kisheria.
Kwa upande wake naibu waziri wa afya maendeleo ya
jamii jinsia wazee na watoto Mh Faustine Ndugulile amesema kuwa ukatili wa
kijinsia hufanyika katika ngazi ya familia na kuitaka jamii kutoifumbia macho
vitendo hivyo kwani serikali inaendelea kuwachukulia hatua watu kama hao.
Hata hivyo bunge la 11 mkutano wa 11 na kikao cha
tatu linaendelea mjini Dodoma ambapo wabunge wanaendelea kujadili bajeti ya
waziri mkuu ya mwaka wa 2018/2019 aliyoiwasilisha siku ya jana.
WAZIRI NCHEMBA AWAOMBA VIONGOZI WA DINI KUWAELIMISHA WAUMINI WAO ILI WAEPUKANE NA UNYANYASAJI.
Reviewed by safina radio
on
April 05, 2018
Rating:
No comments