VYANDARUA LAKI MOJA NA ELFU TISINI VYATOLEWA ZANZIBAR.


 Zaidi ya Vyandarua laki moja na elfu tisini vimetolewa katika vituo vya afya visiwani Zanzibar kwa watoto wenye umri chini ya mwaka mmoja na kwa wamama wajawazito lengo likiwa ni kumaliza ugonjwa wa malaria ifikapo mwaka 2023.

Image result for PICHA YA VYANDARUA


Waziri wa Afya visiwani Zanzibar Hamad Rashidi wakati akizindua ugawaji wa vyandarua kwa njia ya kuponi Mjini Unguja amesema kuwa asilimia sabini ya Wazanzibar ndio wanaotumia vyandarua huku lengo la Shirika la afya Duniani WHO likiwa ni kufikia asilimia themanini na tano.

Aidha amesema kuwa ugawaji wa vyandarua hivyo vilivyopatikana umeshaanza kwa walengwa katika vituo vya afya ambapo amewataka wanufaika hao kuvitumia kwa kufuata maelekezo ya wataalam wa afya.

Hata hivyo, ametahadharisha kwa kusema kuwa serikali itahakikisha vyandarua hivyo vilivyo gawanywa kwa wananchi haviuzwi bali vinatolewa bure pamoja na dawa za malaria.

VYANDARUA LAKI MOJA NA ELFU TISINI VYATOLEWA ZANZIBAR. VYANDARUA LAKI MOJA NA ELFU TISINI VYATOLEWA ZANZIBAR. Reviewed by safina radio on April 05, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.