MAADA BIO ATANGAZWA KUWA MSHINDI KATIKA UCHAGUZI WA DURU YA PILI.


Kiongozi wa upinzani nchini Sierra Leone Julius Maada Bio, ametangazwa na tume huru ya uchaguzi nchini humo kuwa mshindi wa duru ya pili ya uchaguzi wa rais uliofanyika March 31mwaka huu.
Image result for PICHA YA JULIUS MAADA BIO
MAADA BIO
Bw Maada Bio mwanajeshi wa zamani mwenye umri wa miaka 53 ametangazwa baada ya kushinda nafasi hiyo kwa asilimia 51.81 dhidi ya mgombea wa chama tawala Samura Kamara aliyepata asilimia 48.19.
Hata hivyo mgombea wa chama tawala Samaura Kamara amesema atakata rufaa mahakamani kupinga matokeo hayo yaliyotangazwa na tume huru ya uchaguzi ambayo amesema hayakuzingatia malalamiko yake kuhusu dosari zilizojitokeza huku akiwatolea wito wafuasi wake kusalia kuwa watulivu na wenye mshikamano.
Wakati huo huo, Kelele, vifijo na Nderemo vimesikika jana usiku wakati mwenyekiti wa tume huru ya uchaguzi Nec Mohmaed Conteh alipotangaza matokeo hayo.
Saa mbili baada ya kutangazwa kwa matokeo hayo, Julius Maada Bio alikula kiapo pia na kukabidhiwa madaraka kutoka kwa mtangulizi wake Ernest Bai Koroma ambaye alishinda katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2012.

MAADA BIO ATANGAZWA KUWA MSHINDI KATIKA UCHAGUZI WA DURU YA PILI. MAADA BIO ATANGAZWA KUWA MSHINDI KATIKA UCHAGUZI WA DURU YA PILI. Reviewed by safina radio on April 05, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.